Skip to main content

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

     

 ISAYA 28:13
"Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......"

Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu
Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo.

HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI:
Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi
{ i } Ni kuomba
Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako.

{ ii } Ni Mungu kusikia maombi yako.
Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi.

{ iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako.
Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yako.

{ iv } Ni Mungu kukujibu.
Mungu akishamaliza kutafakari maombi yako hatua inayofuata ni yeye kuyajibu maombi hayo.
Naamini katika hatua hizi za maombi kupitia umenielewa. Usije ukafikiri kwamba ukiomba tu Mungu atajibu maombi yako hapana ni mpaka asikie kisha atafakari hayo maombi, kisha ndipo sasa akujibu haleluyaaaa.
    MATHAYO 7:7-8
"Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa;

👉Nataka ujue kwamba tatizo la kutojibiwa maombi yako haliko kwa Mungu bali liko kwako mwenyewe unayeomba kwa sababu ya kutokujua KANUNI za Mungu za kuomba.

 Kuna vitu ambavyo vimejificha hutaweza kuvipata mpaka umevitafuta wewe kwa njia ya maombi. Na kuna mambo yako maishani mwako ambayo yamefungwa kwahiyo hayataweza kufunguliwa mpaka umebisha kwa Mungu kwa njia ya maombi.
Sasa ngoja nikupitishe kwenye hizo kanuni chache,

KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA:

1 Muombaji sharti usiwe mwenye dhambi.
    YOHANA 9:31
"Tunajua kwamba Mungu HAWASIKILIZI watu wenye Dhambi, ila humsikiliza yeyote mwenye kumcha na kutimiza mapenzi yake" ( Tafsiri ya Habari Njema )
👉 Umeona kwamba Neno la Mungu limeweka wazi kabisa kwamba unapokuwa mwenye dhambi Mungu hatakusikiliza kabisa wakati unamuomba. Kwahiyo ili Mungu ajibu maombi yako ni lazima uishi maisha ya Utakatifu, achana na kufanya dhambi kwa siri/kujificha.

2 Muombaji sharti ukae ndani ya kristo Yesu.
    YOHANA 15:7
"Ninyi MKIKAA Ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, Ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"
👉 Mungu hawezi kuyajibu maombi yako kama wewe hujakaa ndani ya Yesu Kristo. Ninaposema kukaa ndani ya Yesu Kristo maana yake nilazima Uokoke sawa.

3 Muombaji sharti Uombe kwa Bidii sana.
   YAKOBO 5:17
"Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, AKAOMBA kwa BIDII mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita"
👉 Eliya aliomba kwa bidii sana kuhusu mvua kutonyesha na Mungu akajibu hayo maombi yake.
   MATENDO 12:5
"Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa LIKAMWOMBA Mungu kwa JUHUDI/BIDII kwa ajili yake"
👉 Hapa tunaliona kanisa likimuombea kwa bidii Petro wakati alipokamwatwa na mfalme Herode na kutokana na kanisa kuomba kwa bidii Mungu alisikia maombi yao akawajibu na kumtoa Perto ndani ya gereza.
👉 Kuomba kwa bidii maana yake ni kuomba bila kukata tamaa aidha kwa kukatishwa na wanadamu au mazingira.
Huwa ili Mungu ajibu maombi yako  ni lazima aione bidii yako wakati unaomba, lakini ukiomba kwa ulegevu hawezi kukujibu.


➡ Kwa sasa hivi naishia hapa katika kanuni hizo ila baadae nitakueleza kanuni nyingine.
Mimi ni rafiki yako Mtumishi Samweli Kibiriti
Utanipata kwa simu namba 0765 867574 na tigo ni 0673 784197 namba zote ziko WhatsApp.
Mungu akubariki sana.

Comments

  1. Asante sana kwa hatua hizi mhimu za maombi,kuna kitu nimepokea.
    Mungu akubariki sana.

    ReplyDelete
  2. Akika Ni kipindi kizuri Mungu akuinue zaid

    ReplyDelete
  3. NAOMBA kuunganishwa na group la whatsp 0629344312

    ReplyDelete
  4. Ameeni nimekuelewa sana nanimejifunza

    ReplyDelete
  5. Naomba kuunganishwa na group hili la whatsp

    ReplyDelete
  6. MUNGU akubarik pastor na kukuinua katika viwango vingne

    ReplyDelete
  7. Naomba kuungwa kwa group la kufundiaha neno la MUNGU 🙏🙏

    ReplyDelete
  8. Halo watu wote, jina langu ni Marvelyn Larry. Kwa muda mrefu, mume wangu alikuwa akiishi katika ghorofa nyingine kutokana na shinikizo la kazi na tulifurahi sana pamoja ingawa alikaa mbali nasi kwa miezi kadhaa. Sikujua mwenzangu wa kazi tayari alikuwa na uhusiano naye jambo ambalo lilimfanya mume wangu anipe talaka bila kutarajia. Nilijua kuna kitu kibaya kwa sababu hatukuwahi kupigana au kubishana kiasi hicho ili kumfanya aondoke. Nilikuwa na kiwewe na natafuta msaada wa kukabiliana na hali hiyo iliyonipeleka kwa DR DAWN kutokana na sifa walizomwagiwa na watu mtandaoni. Tulizungumza kwa kirefu na aliniambia kila kitu nilichohitaji kujua kuhusu kile kilichotokea na utaratibu unaofaa wa kurekebisha matatizo. Alitimiza ahadi zake na kumrudisha mume wangu kwangu na mchakato wa talaka ukafutwa. Sasa mume wangu amerudi nyumbani kwetu na tuna furaha pamoja. Inashangaza sana jinsi watu wanaweza kusaidia watu wengine wakati wanahitaji. Anaweza kukusaidia pia. Mtumie tu ujumbe kupitia WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete

Post a Comment

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers