Skip to main content

Posts

Showing posts from March 24, 2016

MANENO MANNE(4) YANAYOWEZA KUKUZA IMANI YAKO

1- LUKA 1:37 " Kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu" Tambua kua hakuna kinachomshinda Yesu, jambo unaloona ni gumu mnoo kwa Mungu ni dogo sana. , 2- ISAYA 49:15   " Je mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyae, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe" Tambua hata kama unapitia magumu kivipi Mungu hajakusahau na kama alivowakumbuka wana wa israel atakukumbuka. 3- EZEKIEL 37:5     " Bwana Mungu aiambia mifupa hii maneno haya, tazama nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi" Kama kuna chochote kimekufa kwenye maisha yako basi ujue kinaweza kufufuka maana kama Mungu aliweza kutia pumzi na kuipa uhai mifupa mikavu, basi hilo jambo unalosumbuka nalo ni dogo sana ndugu muamini Mungu atakuinua na kukufikisha ulipokusudiwa. 4- YOHANA 14:13     " Nanyi mkiniomba lolote kwa jina langu, hilo nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya mwana"   Ni nafasi ya kipekee kila mkristo amepewa kua ...

IMANI YA NAMNA HII LAZIMA UPATE MAJIBU

Waebrania 11-1 "basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo,ni bayana ya mambo yasiyoonekana" Imani inakupa kuamini kama Mungu yupo kwasababu hamna ambaye ameshamuona MUNGU   Imani inafanya muujiza kutokea kwako,usipokua na imani hutopokea muujiza wako Imani inasababisha wewe kwenda mbele, watu wengi wanajizuilia kupokea kwa kuangalia mazingira yao..Jaribu unalopita nalo lisikutoe kwenye kusudi lako.   Kama huna imani hutompendeza Mungu Mungu hufanya makao kwa mtu mwenye imani Kipimo cha imani ni upendo [ ukimpenda Mungu utafanya yale anayosema .] Imani ndo inamfanya mtu asitende dhambi kwasababu anaamini Mungu hapendezwi na dhambi. Upendo wako kwake unakufanya ufanye lolote ili umfurahishe. Ukiwa tayari kutumika na Mungu,Mungu atakutumia Mfano:unamuomba Mungu akupe gari lakini hujui kuendesha Mtu mwenye imani atachukua hatua ya kwenda kujifunza kwa sababu ana amini Mungu atampatia gari.

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

Total Pageviews

Followers