Skip to main content

NJIA TANO ZAKUFANIKIWA

Bwana asifiwe,
Kila mtu anapenda kufanikiwa, lakini tatizo limekua ni namna gani ambavyo mtu unaweza kufanikiwa.
Leo nmewaandalia njia tano ambazo wewe mkristo ukifuatilia lazima uone mafanikio.

Unatakiwa ujue mambo haya kwanza kabla hujafikiria jinsi ya kufanikiwa

  • Ni mapenzi ya MUNGU kuona wewe unafanikiwa
3 YOHANA 1:2
"Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kua na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo"

  • Ni MUNGU pia anayekupa nguvu za kuweza kufanikiwa
 KUMBUKUMBU LA TORATI 8:18
"Bali utamkumbuka BWANA ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako kama hivi leo"
 Baada ya kufahamu hayo sasa basi tutakwenda kuona ni vitu gani ambavo vinaweza kumfanya mkristo afanikiwe kwa kupitia mifano halisi kwenye neno la MUNGU.


    1.  KUISHI VIZURI NA MUNGU
Jinsi utakavoishi na kumpendeza MUNGU ndivo MUNGU atakapo kukubariki na kukuongeza zaidi na zaidi.
ZABURI 1:1
"  Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
2  Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
3  Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa."

Tunaona kabisa kua ambaye atafuata sheria za BWANA ndo atakaefankiwa kwa kila atendalo. Tusiwe watu wa mizaha wala tusifuate mashauri ya wasio haki pia tupende kutafakari neno la MUNGU na kufanya yale yote MUNGU ametuamuru tufanye.

  2.  KUISHI VIZURI NA WATU
Watu wengi wameshindwa kufanikiwa kwa sababu ya kua na mahusiano mabaya na jamii yao. Wengi hata maofisini hawapandishwi vyeo kwasababu ya kua na mahusiano mabaya na wafanyakazi wenzako.
1 SAMWELI 18:14-16
" 14  Naye Daudi akatenda kwa busara katika njia zake zote naye Bwana alikuwa pamoja naye.
15  Sauli alipoona ya kwamba alitenda kwa busara sana, yeye alimwogopa.
16  Lakini Israeli wote na Yuda wakampenda Daudi; kwa kuwa alitoka na kuingia mbele yao" 

Tunaona jinsi Daudi alivoishi na watu vizuri mpaka sauli akaogopa maana alijua atachukua ufalme, hivyo kuishi kwetu vizuri na watu kuna tupa nafasi nzuri ya kufanikiwa maana huwezi kujua huyo ambaye unasema adui yako leo hujui kesho anaweza kua wa msaada gani kwako.

3.  MTUMIKIE MUNGU.
Pia unaweza kufanikiwa kwa kumtumikia MUNGU kwa uaminifu. Unaweza kumtumikia MUNGU kwa njia tofuati, kuleta watu kwa YESU ni utumishi jitahidi kumtumikia MUNGU kwa njia hiyo ya kuleta watu kwake maana mtu mmoja akimpokea YESU huko mbinguni kunasherekea.
AYUBU 36:11
 "11  Kama wakisikia na kumtumikia, Watapisha siku zao katika kufanikiwa, Na miaka yao katika furaha."

4. AMANI
Amani ni muhimu mno, shetani ili aweze kupata mlango wa kukuingilia lazima avuruge amani yako, jitahidi ue na amani wakati wote usiruhusu huzuni moyoni mwako.
ZABURI 122:6
" 6  Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao"

Pia tunaweza kuona jinsi amani ya ayubu ilivotoweka shetani ndo akapata mlango wa kumuingilia
AYUBU 3:26
"26  Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu"

5. IMANI
Ukiwa ni mtu wa imani ziku zote utampendeza MUNGU, kwahio ukimuamini MUNGU kua anaweza kukufanikisha basi atakufanikisha.
MATENDO YA MITUME 16:30
" 30  Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako."

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers