Skip to main content

SILAHA ZA VITA VYA ROHONI PART ONE

 
Bernard Steven

Bwana YESU atukuzwe wapendwa
Napenda tujifunze jambo ambalo litaponya na kutueka huru
Biblia inasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa
Basi usipitwe na maarifa haya.
Tambua kua Mungu hasemi kitu kwa sababu kina ukweli bali neno lake ni kweli.
Na pia biblia inasema utaijua kweli na kweli utakueka huru, kwahio anaetaka kua huru basi soma hili somo ujifunze jambo upate maarifa na ulitendee kazi.
Nataka tujifunze kuhusu vita vya mkristo.
Tunatambua kua vita vyetu si vya mwilini bali ni vya rohoni.
Sentensi hio yawezekana umeisema sana kwa kinywa chako au umeisikia watu wakisema lakini usielewe wanamaanisha nini.
Wengi tunatamka kwa kinywa kua vita vyetu ni vya rohoni lakini kiuhalisia unapigana vita hivo kimwili.
Wengi tumekua tukikerwa kidogo tu unagomba kweli na unajibizana na mtu aliekukera afu unasema unapigana vita vyako kiroho.
Mtu kakutukana una mjibu na wewe afu unasema vita vyako unapigana kiroho.
Umesingiziwa uongo unalalamika kwa kila mtu unasema wamekuonea afu unasema vita vyako vya kiroho
Hapana kabisa vita vya kiroho hatupigani namna hio.
Wakikusema,wakikutukana,wakikuonea ingia chumbani mwako piga goti tamka msamaha kwa hao watu muachie Bwana.
Kama mtoto wako mtundu mkabithi Yesu ashuhulike na tabia yake hivo ndo tunaishi sisi tulio rohoni.
Ila pia inawezekana kweli unapigana vita kiroho lakini umevaa silaha chache za kwenda katika hio vita ya kiroho.

Waefeso 6:11"Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani."

Kuna silaha ambazo ukizivaa rohoni hio vita lazima ushinde
Silaha za Vita
Katika vita hivi vya kiroho tunaitaji silaha.
Sasa utauliza tunavaaje hizo silaha wakati vita ni rohoni.
Hata silaha zenyewe unazivaa kwa namna ya rohoni.
Unachotakiwa ni kujua ni namna gani unavoweza kuvaa silaha zote.
Silaha ndo kama zifuatazo

Waefeso 6:14-17"Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,   na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;"


1-MKANDA-KWELI

Mkanda siku zote unamfanya mtu kua huru bila vazi alilovaa kumsumbua
Hivyo kama Mkristo lazima avae mkanda ambao hutokana na kuishi katika kweli.
Ili uweze kua na hii silaha kama mwanajeshi wa Kristo tembea kwenye ukweli

Yohana mtakatifu 8:32"tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru".

Kristo ndio kweli (Ukitembea na Kristo umetembea katika ukweli)
Tukiwa na kweli tutakua huru ndio sifa ya mkanda kukufanya uwe huru katika shughuli zako.

Yohana 17:17" Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli." 

Mstari huu unaongelea kuhusu kutakaswa na kweli, afu pia inasema kweli ni neno na pia tunajua neno ndio Kristo mwenyewe.

YOHANA 1:1-3"Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.  Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika". 

 

Huo mstari unamuongelea Kristo kua ndio neno

 

Yohana 14:6"Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi."

 

Inathibitisha kua kweli yenyewe ndio Kristo

2-DIRII-HAKI

Wengi hujiuliza haki ni nini, biblia inaposema haki ina maanisha kitu gani?
Haki kwa tafsiri ya Biblia ni kutokua na aina yeyote ya uovu wala dhambi au kwa lugha nyingine mtu asie tenda dhambi ndio anahesabiwa kua ni haki.

Warumi 9:30 "Tuseme nini, basi? Ya kwamba watu wa Mataifa, wasioifuata haki, walipata haki; lakini ni ile haki iliyo ya imani"

Tukisoma hapo juu iinatudhihirishia kua haki ni kitendo cha kutokua na dhambi
Maana tunajua Yesu alikufa msalabani ili sisi tulio na dhambi tusamehewe maovu na tuwe na haki mbele za Mungu.

Zaburi 37:21"Asiye haki hukopa wala halipi, Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu"

Inatoa tofauti kati ya mwenye haki na asiye na haki
Mwenye haki hupenda kutenda mema bali asiye na haki hufanya matendo yote ya kuzulumu na yasio mema.

 Mithali 21:21"Aandamaye haki na fadhili, Ataona uhai na haki na heshima".

Pia haki ina uzima wa milele bali asiye na haki hana uzima wa milele bali mauti

1Yohana 3:7  "Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki"

Siku zote atendaye haki atapata haki kwasababu anaenenda katika mapenzi ya Mungu lazima Mungu amuonekani kwa namna ya kipekee.

Kwa sasa nitaishia hapa ila kwa sasa tafakari haya mkiyangojea maendelezo yatayokuja  hivi karibuni,
ila tutambue kua hizi silaha huwezi kuzivaa kama hujamkabithi YESU maisha yako, ebu leo chukua uamuzi wakuokoka ili uweze kumfurahia huyu YESU wetu kwa pamoja.

SOMA SALA IFUATAYO KAMA UKO TAYARI KUOKOKA

BWANA YESU,NAJA KWAKO (MIMI) KAMA NILIVYO,NIMETAMBUA YA KWAMBA MIMI NI MWENYE DHAMBI.NIMETAMBUA YA KWAMBA NI WEWE TU UNAYEWEZA KUNISAMEHE NA KUNITAKASA.NAOMBA UNISAMEHE DHAMBI ZANGU ZOTE. NAOMBA ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,NA KULIANDIKA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE. NAYAKABIDHI MAISHA YANGU KWAKO,UNILINDE NA MWOVU SHETANI. NAJITOA KWAKO KUANZIA LEO/SASA,UNIFANYE KUWA KIUMBE KIPYA NA UNITUMIE KAMA UPENDAVYO. AHSANTE KWA KUNIKUBALI AMEN.

Contacts
Email:ste.bernard@yahoo.com
Phone no:0659447445

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers