Skip to main content

DHAMBI MOJA HUVUTA NYINGINE NA KUMFANYA MTENDAJI AENDELEE KUZAMA

Bwana Yesu atukuzwe?

Dhambi ni tendo lenye mvuto mkubwa ambapo mtu anapoitenda moja huvuta kiu fulani na kumpelekea mtu yuyo huyo kuitenda dhambi nyingine.

Shetani ni mshawishi mkuu wa kukutumbukiza kwa dhambi moja kwenda nyingine kwani atakuchochea uibie rafiki yako leo na ukifaulu atakuja tena kesho akukumbushe jana akwambie uirudie dhambi ile ya jana maana hakuna mtu alikuona.

Wakati huo utakuwa unasikia sauti ndogo ya kukunong'onezea ikikwambia: "Enda uregeshe kile ulichoiba jana na usirudie kuiba tena leo" Sauti hii inaweza kuwa ni wazo kwa akili yako kisha ukiitii huwa umempendeza Mungu wa mbinguni.

Unapofanya uzinzi/ uasherati na mwenzako, dakika moja baada ya tendo utasikia sauti fulani ikikuhukumu na kukuuliza kwanini umefanya uovu huu? Sauti hii ndio iitwayo Roho wa Mungu inayokuhukumu ukifanya dhambi na inakutaka utubu na kuacha kabisa dhambi hiyo.
Leo Mungu kupitia Roho wake amenituma nikwambie kuwa kuna kitu cha mtu umechukua na unajua vizuri kuwa sio chako.
Kuna mke wa mtu una-push naye na huku unajua kuwa ni mali ya mtu, Mungu anasema uache na utubu atakusamehea.
Kazi hizi unazozifanya ni za kishetani bali Yesu hataki huzifanye ila anakutaka ubadilike leo.
Kuna mume wa mtu unaishi naye kimapenzi huku mkewe analia kwa shida na kukosa upendo, Mungu ameniambia uache tabia hiyo kisha utubu. Yesu Kristo alikuja duniani kuvunja dhambi kama hizi na anatutaka tuache kabisa uovu huu.
1Yohana 3:8b
"Kwa maana mwana wa Mungu alidhihirishwa ili kuzivunja kazi za shetani"
Mkatae shetani na hila zake za kukunasa na dhambi moja hadi nyingine na umwendee Bwana Yesu siku ya leo.
Mtu aliye na masikio asikie sauti ya Yehova Mungu wa mbinguni na kuitii sauti yake.
Ubarikiwe kwa kuyasoma makala haya pia kama haujamkabidhi Bwana Yesu maisha yako, hakikisha umefanya hivyo sasa.

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers