Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho.
{ Sehemu ya pili }
Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na
kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni
muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako
kujibiwa haraka na Mungu.
KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA:
4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.
4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.
YOHANA 15:7
"Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"
"Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"
WAKOLOSAI 3;16
"Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"
"Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"
YEREMIA 1:12
"Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize"
"Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize"
Kwahiyo hakikisha ndani ya moyo wako umelijaza Neno la
Mungu na unapofanya maombi uyafanye katika msingi wa Neno la Mungu sawa.
5 Muombaji sharti uwaombee watu wengine.
AYUBU 42:10
"Kisha BWANA akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo ALIPOWAOMBEA rafiki zake; BWANA naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza"
"Kisha BWANA akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo ALIPOWAOMBEA rafiki zake; BWANA naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza"
Tafsiri ya Neno Biblia inasema "Baada ya Ayubu KUWAOMBEA
rafiki zake, BWANA akamfanikisha tena naye akampa mara mbili kama yale
aliyokuwa nayo hapo kabla"
▶ Hapa Biblia inatueleza kwamba baada ya Ayubu kuwaombea
kwa Mungu rafiki zake Mungu akageuza uteka wake na kumfanikisha mara
mbili zaidi.
6 Muombaji sharti uombe kwa kutumia Jina la Yesu Kristo.
YOHANA 14:13-14
"Nanyi mkiomba lo lote kwa JINA LANGU, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. MKINIOMBA neno lo lote kwa JINA langu, nitalifanya"
"Nanyi mkiomba lo lote kwa JINA LANGU, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. MKINIOMBA neno lo lote kwa JINA langu, nitalifanya"
YOHANA 16:23-24,26
"Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote, Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa Jina langu. Hata sasa hamkuomba neno kwa JINA LANGU; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu. Na siku ile mtaomba kwa JINA langu......."
"Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote, Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa Jina langu. Hata sasa hamkuomba neno kwa JINA LANGU; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu. Na siku ile mtaomba kwa JINA langu......."
7 Muombaji sharti umpatie heshima Roho Mtakatifu katika maombi yako.
WARUMI 8:26-27
"Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka. Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na Mapenzi ya Mungu" ( Tafsiri ya Habari Njema )
"Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka. Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na Mapenzi ya Mungu" ( Tafsiri ya Habari Njema )
YOHANA 14:26
Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia"
Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia"
➡ Wako watu wengi ambao wakitaka kuingia kwenye maombi huwa
hawamshirikishi na kumpa heshima anayoshahiri Roho Mtakatifu. Huwa wao
wanaona kwamba ni wataalam wa kuomba bila kujua kwamba Biblia imeweka
wazi kabisa kwamba hakuna mtu anayejua kuomba ipasavyo na sawasawa na
mapenzi ya Mungu bila msaada wa kuongozwa na Roho Mtakatifu.
Nataka utambue kwamba Roho Mtakatifu ili akusaidie kuomba sawa sawa na
mapenzi ya Mungu nilazima utambue kwamba yuko na ametumwa duniani
kutusaidia pia ni lazima umpe heshima yake,
Ninaposema umpe heshima yake namaanisha nini? maana yake nikwamba kabla hujaanza kuomba mwambie "Roho Mtakatifu najua kwamba upo na umetumwa duniani kwaajili yangu nakuomba uniongoze katika haya maombi yangu na uniombee kama vile apendavyo Mungu sawasawa na mapenzi yake, karibu tuombe pamoja katika Jina la Yesu Kristo" Ukishatamka hivyo tayari Roho Mtakatifu anajua kuwa unaheshimu msaada wake na uko tayari akufundishe jinsi ya kuomba na kukuongoza na kukusaidia.
Ninaposema umpe heshima yake namaanisha nini? maana yake nikwamba kabla hujaanza kuomba mwambie "Roho Mtakatifu najua kwamba upo na umetumwa duniani kwaajili yangu nakuomba uniongoze katika haya maombi yangu na uniombee kama vile apendavyo Mungu sawasawa na mapenzi yake, karibu tuombe pamoja katika Jina la Yesu Kristo" Ukishatamka hivyo tayari Roho Mtakatifu anajua kuwa unaheshimu msaada wake na uko tayari akufundishe jinsi ya kuomba na kukuongoza na kukusaidia.
8 Muombaji sharti uwe mtii wa maagizo ya Neno la Mungu.
ISAYA 1:19
"Kama mkikubali na KUTII mtakula mema ya nchi"
"Kama mkikubali na KUTII mtakula mema ya nchi"
⚡ Kuna tofauti ya kukubali na kutii. Unaweza ukakubali Neno
la Mungu( Biblia ) lakini usitii maagizo ya Neno la Mungu kwahiyo
nilazima uikubali Biblia na vitabu vyake vyote kuanzia Mwanzo mpaka
Ufunuo kisha uyatii maagizo yote ambayo Mungu ameyaelekeza ndani ya Neno
lake ( Biblia )
KUMBUKUMBU LA TORATI 28:1
"Itakuwa utakaposikia Sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa Bidii, kutunza kuyafanya Maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani"
"Itakuwa utakaposikia Sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa Bidii, kutunza kuyafanya Maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani"
⏩ Sasa kwa muda huu naomba niishie hapa katika kanuni hizi
baadae nitamalizia kanuni nyingine ambazo Mungu amejiwekea ili aweze
kujibu maombi ya wanadamu wanayomuomba.
➡ Kama utahitaji maombi au ushauri utanipata kwa mawasiliano haya simu 0765 867574 na tigo ni 0673 784197, kwa Email ni Samwelikibiriti@gmail.com
Mimi ni rafiki yako Mtumishi Samweli Kibiriti
Mungu akubariki kwa kujifunza somo hili
I'm blessed..... Thank you
ReplyDeleteUbarikiwe sana Mwalimu
ReplyDeleteNaomba mniunge kwenye group hili la WhatsApp
ReplyDeleteHalo watu wote, jina langu ni Marvelyn Larry. Kwa muda mrefu, mume wangu alikuwa akiishi katika ghorofa nyingine kutokana na shinikizo la kazi na tulifurahi sana pamoja ingawa alikaa mbali nasi kwa miezi kadhaa. Sikujua mwenzangu wa kazi tayari alikuwa na uhusiano naye jambo ambalo lilimfanya mume wangu anipe talaka bila kutarajia. Nilijua kuna kitu kibaya kwa sababu hatukuwahi kupigana au kubishana kiasi hicho ili kumfanya aondoke. Nilikuwa na kiwewe na natafuta msaada wa kukabiliana na hali hiyo iliyonipeleka kwa DR DAWN kutokana na sifa walizomwagiwa na watu mtandaoni. Tulizungumza kwa kirefu na aliniambia kila kitu nilichohitaji kujua kuhusu kile kilichotokea na utaratibu unaofaa wa kurekebisha matatizo. Alitimiza ahadi zake na kumrudisha mume wangu kwangu na mchakato wa talaka ukafutwa. Sasa mume wangu amerudi nyumbani kwetu na tuna furaha pamoja. Inashangaza sana jinsi watu wanaweza kusaidia watu wengine wakati wanahitaji. Anaweza kukusaidia pia. Mtumie tu ujumbe kupitia WhatsApp: +2349046229159
ReplyDeleteBarua pepe: dawnacuna314@gmail.com