Skip to main content

MSAMAHA

Bwana asifiwe wapendwa,

Unapoishi na wanadamu kukosana kupo,

Nikama glasi kwenye kabati zinazo kaa pamoja huwa hazikosi kugongana ...ndivo na binadamu wakaao pamoja amnavyo hawakosi kuhitilafiana

Pengine MUNGU ana maana yake ,wewe ukosewe,uachiliea MSAMAHA, ili nayeye akuchukue viwango fulani vya juu kwa sababu tu umetii agizo lake juu ya MSAMAHA.

KUSAMEHE NI AGIZO LA MUNGU

>Samehe saba Mara sabini
Luka  17: 4 " Na kama akakukosa Mara saba katika siku moja,na kurudi kwako Mara saba akisema nimetubu samehe.

>Ukisamehe utasamehewa
Mathayo  6;14-15

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao,na Baba wenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.

Bali msipowasamehe watu makosa yao,wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

>Samehe kama ulivyosamehewa

Kumbuka waliotutangulia (Adam na Hawa) walivunja mzizi wa utii ,wakatuingiza kwenye mkumbo wa uovu.....

Warumi 3: 23-24
" kwa sababu wote wamefanya dhambi na kupungukiwa utukufu wa MUNGU

Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake,kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.

Waefeso 4:32
Tena  iweni wafadhili ninyi kwa ninyi,wenye huruma mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi"

TAFSIRI YA MSAMAHA HASA NI IPI ?

Kusamehe ni tendo la moyoni wala si kinywani au usoni linalokupa kujigharimu kurudisha mahusiano yaliyopotea

Kusamehe ni hali yakujishusha au kujinyenyekeza au kujitoa kwa gharama yoyote ile ili tu kuhakikisha umerudisha mahusiano yaliyopotea

Kurudisha mahusiano yaliyopotea siyo kazi rahisi. Unaweza ukakuta mwenzako anapanga kukuua, anapanga kuchoma moto nyumba yako,anapanga kukuchongea au kukusakizia balaa Fulani kwa sababu tu ya uhasama.

Akawa yeye nafsi yake imedhamiria kwa asilimia zote akufanyie baya . hakuongeleshi wala kukusalimia, akikuona barabara kuu yeye anakata uchochoroni, hataki hata kukuona wala
kukusikia.

Je UNAFIKIRI hapo mlipofikia nikazi rahisi?

Huwa inafikia hatua mahusiano kurudi yakahitaji gharama kubwa sana.

MSAMAHA siyo agizo la hiari bali ni agizo la lazima la MUNGU kwa mwanadamu. UKILIPUUZIA HUTOBAKI SALAMA

Kwa mfano. Unaweza kukuta mwingine alishakosana nawazazi wake na alishaapa hatokuja kuwasamehe wazazi wake hata iweje.

MUNGU anasema mtu wa namna hiyo hatabaki salama kupitia maandiko yake matakatifu

Mithali 20:20
"Amlaniye babaye au mamaye taa yake itazima katika Giza KUU"

WAEFESO 6:2-3
 
Waheshimu baba yako na mama yako,amri hii ndiyo ya kwanza yenye ahadi.

Upate heri ukae siku nyingi katika dunia

Kutoka 20:12

Waheshimu baba yako na mama yako ,siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA,Mungu wako .

"NIMEKUSAMEHE lakini SITAKUSAHAU"

Je,ungekuwa wewe ukasikia kauli hii kwa mshitaki wako utaipokeaje????

MUNGU atutie nguvu tukikutana tena tuiangalie kauli hii. Ukweli wake hasa ni upi

           Ahsanteni

               By

Silas Mayayz.

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers