Skip to main content

NAWAPENDA WALE WANIPENDAO NA WENYE KUNITAFUTA KWA BIDII WATANIONA

Bwana Yesu asifiwe sana

Kichwa cha ujumbe huu nimekitoa kwa Biblia:

Mithali 7:18
"Nawapenda wanipendao na wenye kunitafuta kwa bidii wataniona".

Hii ni sauti ya Bwana Mungu akituelezea upendo wake kwetu.
Ni vigumu hata kwa maisha ya kibinadamu kumpenda asiyekupenda.

Ili upendwe ni lazima mwenyewe uwe unapenda kwa maana upendo haulazimishwi na uwezi kupendewa na mtu mwingine.

Ili Mungu akupende ni lazima uonyeshe dhana ya kumpenda kupitia njia tofauti.

Ili umpate Mungu ni lazima umtafute na sio kumtafuta pekee ila umtafute kwa bidii ndio umuone.

Kumbuka watu wanaomtafuta Mungu duniani ni wengi sana hivyo unahitajika kumtafuta kwa bidii sana ndio umpate.

Unapomtafuta Mungu ujue kuna mamilioni pia wanamtafuta Mungu yuyo huyo na na unahitajika utie bidii zaidi ili uwe wa kwanza kumuona.

Mungu mwenyewe ni Roho na ndio umuone ni lazima uwe na macho ya kiroho.

NJIA ZA KUMTAFUTA MUNGU WA MBINGUNI

Kuna njia tano za kumtafuta Mungu wa mbinguni ili umuone ndani ya maisha yako.Njia hizi ni:

1.Kutubu,kuacha dhambi na kuokoka.

2.Kuishi maisha ya maombi mengi ndani ya imani ya Bwana Yesu.

3.Kutoa sadaka/zaka/fungu la kumi.

4.Kumpa Mungu maisha yako yote kwa utumishi wa kazi take pasipo kutarajia chochote kama malipo.

5.Kulisoma na kulitii Neno la Mungu wa mbinguni huku ukienda ibada Kanisani.

Kama umekuwa ukimtafuta Mungu na bado haujamuona kwa kutimiza haya ujue unamtafuta Mungu ila haumtafuti kwa bidii.
Ndani yako tia bidii utaona mabadiliko baada ya kuutii ujumbe huu.

Watu wengi wanaenda Kanisani wakisema wanamtafuta Mungu na huku hawajasimamia wokovu.

Mungu anataka usimamie wokovu kwa ukweli.

Watu wengi wanatangaza mbinguni wao wenyewe wasioienda kwani wamejawa na unafiki huku wakisema wanamtafuta Mungu wa mbinguni.

Itakuwa ni aibu mpendwa mimi Geoffrey ninatumia muda mwingi nikihubiri injili nikose kuingia mbinguni huku niliowahubiria wakienda mbinguni.

Tubu dhambi zako leo mimi nimetubu zangu mpendwa tumtafute Mungu na tutamuona.

Ndio upone huo ugonjwa, hiyo hali mbaya ikuachie, wahitaji kutubu dhambi zako leo mpendwa kwa Bwana Yesu akuokoe.

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers