Skip to main content

SILAHA ZA VITA VYA ROHONI PART TWO

 
BERNARD STEVEN

Bwana YESU asifiwe,
Napenda kuendelea na mwendelezo wa somo letu la silaha za vita vya rohoni,
tumeshaangalia silaha mbili sasa leo naendelea na silaha ya tatu na kuendelea,
neno tunalo simamia ni:-

waefeso 6:14-17

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu

 

3-Kufungiwa utayari katika miguu

Miguu isiyokua tayari kwenda sehemu mwili huwezi kwenda, miguu ni sehemu muhimu kwa mwanadamu kwani mawazo huanza kwenye ufahamu lakini ili mawazo yako yatimie lazima uchukue hatua.
vivyo hivyo sisi tuliofanyika wana wa MUNGU ni lazima tuwe na utayar wa kwenda kuhubiri injili kwa mataifa yani kwa wale wasiomjua YESU au wanamjua YESU lakini hawajui uweza wake.

MARKO 16:15

" Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe"

 YESU katuamuru tuende kuihubiri injili kwa kila mtu ili waokoke.
Una rafiki,ndugu,majirani ambao hawamjui YESU ebu chukua hatua nenda kawahubirie injili ya KRISTO.
Kua na utayari wa kutangaza injili ya YESU ni moja ya silaha za vita vya rohoni.

4-Imani-ngao

Kwenye vita ngao husaidia kujikinga na mishale hata na mapanga, ngao yako kama mkristo ni imani.

 WAEBRANIA 11:1

" Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana."

Kupitia hapo tunajua kua imani ni kua na uhakika wa jambo ambalo liko mbele na hujaliona lakini una amini litakuwa.
ila tutambue sio kila ila imani ni imani sahihi, imani sahihi na hakika ni ya kumuamini YESU

 WARUMI 10:17

" Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo."

Na imani yenyewe ni moja tu,

WAEFESO 4:5

" Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja."

 

Basi nikupe siri ya imani yako iweze kukua, huzuria ibada na mafundisho ya bible study na usome neno la Mungu
Kiasi cha neno la Mungu ndani yako ndio kiasi cha imani yako, huwezi kuamini zaidi ya ufahamu wako juu ya neno la Mungu.

5-Chapeo-wokovu 

Wokovu ni kitendo cha kukombolewa kwenye dhambi na mauti yake.
Wokovu unapatikana kwa YESU pekee nje ya hapo hamna wokovu.
Wokovu utakusaidia hata ukianguka kiroho uweze kurudi na kuanza safari na YESU.
chapeo ndio helmet yako inayokuzuia ukianguka uwe salama.

6-Upanga wa ROHO- Neno la MUNGU 

WAEBRANIA 4:12

" Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo"

 Neno la MUNGU lina nguvu na uwezo wa kujua mawazo ya mwanadamu, linauwezo wa kumbadilisha mwanadamu,linauwezo wa kumshinda shetani maana hata YESU alimshinda shetani kwa neno.


Natumai umebarikiwa na somo hili la silaha za rohoni.Basi tusiwe wasikiaji wa neno tu bali watendaji, hapo ndo tutaona haya yote niliyo andika humu yakitenda kazi kwa kila mmoja wetu.

Comments

  1. Somo zuri, kwa kuongezea kuna somo pia linaitwa VITA BADO VINAENDELEA...Kulisoma fuata link hii >>https://wingulamashahidi.org/2019/01/31/vita-bado-vinaendelea/...utaongeza maarifa...

    ReplyDelete

Post a Comment

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers