Skip to main content

TALAKA SIO MPANGO WA MUNGU, NI WA SHETANI

Bwana Yesu asifiwe?

Talaka ni mpango wa shetani kuhakikisha kuwa umeishi maisha ya kuishi peke yako ila kusudi la Mungu ni uishi na mke/mume wako.

Baada ya Mungu kumuumba Adamu, aliutoa ubavu wake na kumuumbia mkewe Hawa na Mungu ataitwa mwanamke maana ametolewa kwa mwanamume.

Mwanzo 2:24
" Ndiyo maana mwanamume humwacha baba yake na mama yake akaambatana na mkewe nao wawili huwa mwili mmoja"

Ndoa ilianzishwa na Mungu mwenyewe na hakuianza kwa kusudi la kutalakiana ila ni idumu milele kwani ni kifo pekee chenye ruhusa ya kuitenganisha ndoa.

Ninajua nimekukumbusha mengi kwa ujumbe huu maana ulitalakiwa au kutalakiana ila naomba kukwambia huo haukuwa mpango wa Yehova Mungu wako.

Wengi talaka zao huletwa na uasherati/ uzinzi, ulevi, utasa/ugumba, usingiziaji, kukataliwa na mavyaa/ bavyaa na hata kuyatii mashauri madhaifu ya mchungaji wako ambaye anaweza kuwa ni nabii/mwalimu wa uongo.

Pia najua ninakukumbusha kuwa unaweza kuwa ulichangia kuvunja ndoa ya mtu ila leo nakushauri kwa jina la Yesu ukatubu dhambi hiyo.
Katika maombi nimekuwa nikikutana na watu tofauti wakitaka neno la kinywa la kinabii la kujua kama anayekuoa/ unayemuoa ndiye ubavu wako. Watu hawa huwa na imani yakwamba nitakacho mwambia ndio kweli ya Mungu na mtu huwa tayari hata nikisema siye ubavu waachane ila hapa panahitaji hekima ya Mungu.

Kuna mafidhuli majibwa mwitu wanaopotosha watu wa Mungu kwa kuzivunja ndoa za watu kwa kuchangia kutalakiana huku wakidanganya wametumwa na Yehova Mungu. Ndugu husimwache mkeo/mumeo kwa ushauri mbovu wa mtu yeyote kwani ni laana kwa Mungu na kama ulikuwa umemwacha mumeo/mkeo mrudie leo.

Lisikie Neno la Yehova Mungu wako leo, Mungu anataka umtii na kuokoka ili ukaupate uzima wa milele. Talaka in mpango wa shetani wa:Kuiba,kuharibu na kuyaua maisha yako.

Hakikisha ndoa yako umeianza na kuitanguliza Yehova na itadumu milele.

Hakikisha umeiheshimu ile ya mwenzako kwani mwanzilishi wake pia ni Mungu wa mbinguni na ndiye kiongozi wake.

Kama una masikio nisikie ninavyokwambia kutoka kwa Yehova Mungu wa Israeli.

Kama hujaokoka okoka sasa, Yesu Kristo yu njiani kulitwaa Kanisa lake.

Ubarikiwe na usambaze ujumbe huu kwa marafiki zako.

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers