Bwana Yesu asifiwe?
Talaka ni mpango wa shetani kuhakikisha kuwa umeishi maisha ya kuishi peke yako ila kusudi la Mungu ni uishi na mke/mume wako.
Baada ya Mungu kumuumba Adamu, aliutoa ubavu wake na kumuumbia mkewe Hawa na Mungu ataitwa mwanamke maana ametolewa kwa mwanamume.
Mwanzo 2:24
" Ndiyo maana mwanamume humwacha baba yake na mama yake akaambatana na mkewe nao wawili huwa mwili mmoja"
Ndoa ilianzishwa na Mungu mwenyewe na hakuianza kwa kusudi la kutalakiana ila ni idumu milele kwani ni kifo pekee chenye ruhusa ya kuitenganisha ndoa.
Ninajua nimekukumbusha mengi kwa ujumbe huu maana ulitalakiwa au kutalakiana ila naomba kukwambia huo haukuwa mpango wa Yehova Mungu wako.
Wengi talaka zao huletwa na uasherati/ uzinzi, ulevi, utasa/ugumba, usingiziaji, kukataliwa na mavyaa/ bavyaa na hata kuyatii mashauri madhaifu ya mchungaji wako ambaye anaweza kuwa ni nabii/mwalimu wa uongo.
Pia najua ninakukumbusha kuwa unaweza kuwa ulichangia kuvunja ndoa ya mtu ila leo nakushauri kwa jina la Yesu ukatubu dhambi hiyo.
Katika maombi nimekuwa nikikutana na watu tofauti wakitaka neno la kinywa la kinabii la kujua kama anayekuoa/ unayemuoa ndiye ubavu wako. Watu hawa huwa na imani yakwamba nitakacho mwambia ndio kweli ya Mungu na mtu huwa tayari hata nikisema siye ubavu waachane ila hapa panahitaji hekima ya Mungu.
Kuna mafidhuli majibwa mwitu wanaopotosha watu wa Mungu kwa kuzivunja ndoa za watu kwa kuchangia kutalakiana huku wakidanganya wametumwa na Yehova Mungu. Ndugu husimwache mkeo/mumeo kwa ushauri mbovu wa mtu yeyote kwani ni laana kwa Mungu na kama ulikuwa umemwacha mumeo/mkeo mrudie leo.
Lisikie Neno la Yehova Mungu wako leo, Mungu anataka umtii na kuokoka ili ukaupate uzima wa milele. Talaka in mpango wa shetani wa:Kuiba,kuharibu na kuyaua maisha yako.
Hakikisha ndoa yako umeianza na kuitanguliza Yehova na itadumu milele.
Hakikisha umeiheshimu ile ya mwenzako kwani mwanzilishi wake pia ni Mungu wa mbinguni na ndiye kiongozi wake.
Kama una masikio nisikie ninavyokwambia kutoka kwa Yehova Mungu wa Israeli.
Kama hujaokoka okoka sasa, Yesu Kristo yu njiani kulitwaa Kanisa lake.
Ubarikiwe na usambaze ujumbe huu kwa marafiki zako.
Ushuhuda Wangu wa Kutoka Moyoni 💖
ReplyDeleteBaada ya baba yangu mdogo kuniacha kwa miezi saba mirefu, nilikuwa nimevunjika moyo kabisa. Alinizuia kwenye mitandao yote ya kijamii, akaondoka, na hakukuwa na njia ya kumfikia. Karibu nikate tamaa, lakini ndani kabisa nilijua singeweza kupata mtu yeyote ambaye angenipenda na kunitendea jinsi alivyonitendea.
Siku moja, bosi wangu kazini aligundua jinsi nilivyokuwa na huzuni na akanitambulisha kwa Dkt. Dawn. Dkt. Dawn alisikiliza hadithi yangu na akaahidi kwamba mpenzi wangu angerudi kwangu ndani ya siku tatu. Kwa kweli, sikuamini mwanzoni—lakini kwa mshangao wangu mkubwa, siku ya tatu simu yangu iliita. Ilikuwa yeye! Alikuwa akilia na kuomba msamaha, akisema hataniacha tena.
Tangu siku hiyo, uhusiano wetu umekuwa na nguvu na uzuri zaidi kuliko hapo awali. Amekuwa akipenda na kunijali mimi na mtoto wetu, na sasa tunafunga ndoa katika miezi miwili tu! ❤️
Shukrani zote kwa Dkt. Dawn, ambaye kwa kweli alifanya jambo lisilowezekana liwezekane. Ninampendekeza kwa moyo wote kwa yeyote anayekabiliwa na changamoto katika:
Masuala ya uhusiano au ndoa
Ugonjwa au magonjwa
Matatizo ya utasa au bahati nasibu
Kesi za mahakamani au urejeshaji wa mali
Dkt. Dawn kweli hutatua matatizo kwa ufanisi na hurudisha furaha katika maisha ya watu.
Wasiliana na Dr. Dawn kwenye WhatsApp: +2349046229159
Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com