Skip to main content

JE UNAMJUA MALAIKA WAKO NI NANI?

Bwana YESU asifiwe,
Napenda leo tujifunze kuhusu malaika.

Umesikia sana neno hili malaika, je unajua ni nani huyu malaika?

Basi fuatana na mimi katika hili somo uweze kupata ufahamu wa  malaika ni nani hasa.

NINI MAANA YA MALAIKA?

Kwenye lugha ya kingereza malaika anaitwa "angel" ila hilo neno limetolewa kwenye neno la kigiriki linaloitwa "angelos" ambalo kwa tafsiri yake halisi ya kingereza ni "messenger".
Kutokana na tasfiri hio basi tukija kwenye lugha yetu tunaona kua lina maanisha "mjumbe"

Mjumbe ni yule ambaye amebeba ujumbe wako au wa kitu chochote, kwahio tunapata maana yake kua malaika ni mjumbe kwahio kwa lugha rahisi na nyepesi malaika wako ni yule aliyebeba ujumbe wako.

Ukisoma biblia yako vizuri utaona kua popote malaika alitokea alikua na ujumbe wa mtu.


KUTOKA 23:20-22


"Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake.

Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao."

 

Ni hivi kutokana na hilo neno ukiangalia ufunuo uliopo ndani yake ni hivi:-
  1. MCHUNGAJI
  2. MWALIMU
  3. MTUME
  4. NABII
  5. MUINJILISTI    
Hawa wote kama watumishi walioko mbele zako ambao wamepewa neno la kukufundisha hawa ndio malaika wako.

Ambaye yuko mbele yako kama kiongozi wako wa kiroho ambae MUNGU kamueka mbele yako huyo ni malaika wako.

Ni mjumbe wako maana amebeba ujumbe wako toka kwa MUNGU.

Anaposema anamtuma malaika aende mbele zako anamaanisha atamtuma mtumishi wake aje mbele zako. Akuonyeshe, akufundishe neno la MUNGU ili ujue namna ya kukaa na MUNGU  ili akufikishe kwenye kusudi.
MUNGU anazidi kuhimiza msikilizeni akimaanisha msikilize sana kiongozi wako wa kiroho tii kile anachokufundisha. 

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers