Skip to main content

HATUA KATIKA WITO



Kutoka 3:2

Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.

Yamkini una wito ndani yako na labda unajua kua Mungu amekuita kwa ajili ya kitu fulani.
Mungu akikuita ujue kuna maagizo anataka uyatekeleze, Mungu hatokuita tu ilimradi tu uokoke afu uwe unaenda kanisani na kurudi iishie hapo, kuna zaidi ya hapo, kuna kusudi maalumu kabisa ambalo anataka yeye alifanikishe hapa duniani na ili alifanikishe anaona ni vema akutumie wewe.
Wito sio kua mchungaji,mwalimu,nabii au mtume peke yake
Kazi yako inaweza ikawa wito wako pia.
Kupitia hio kazi Kuna vitu Mungu anataka kuvifanikisha hapa duniani.

Kuna hatua katika wito wako,zifuatazo ndio hatua za kuendea wito wako.

1- KUSHUHUDIA MATENDO MAKUU

Hatua ya kwanza katika Mungu kukutafuta wewe hua anakupa kibali cha wewe kushuhudia matendo makuu yakitendeka mbele ya macho yako,utaona watu wakiponywa,utaona miujiza ya kipekee ambayo hukuwahi kuzani vitu kama hivo vinaweza kutendeka, hii ni hatua ambayo Mungu alitumia kwa musa kwa kutumia kijiti kinachowaka moto bila kutekea huo ulikua ni muujiza unatendeka mbele ya macho yake na yote hio Mungu alifanya ili apate attention ya musa,
Ni wengi sana wamemjua Mungu kutokana na kushudiwa na wao wenyewe kushuhudia matendo makuu ya Mungu yakitendeka ndio Mungu akapata attention yao hii ni kanuni anayotumia Mungu.


2- KUGEUKA


Kutoka 3:3

Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

Hatua ya pili ni kugeuka, dhumuni zima la Mungu kuweka muujiza ni ili kumfanya mtu amgeukie,
Musa aliegeuka akasema ebu nione kwanini hiki kijiti akiteketei, kwahio musa alikua anachunguza yawezekanaje kabisa kijiti hiki kisitekete wakati kinawaka moto, alikua ni mdadisi anatamani kuelewa. Hii ni hatua ya pili kwa mtu ambae Mungu humuita hua anadadisi sana miujiza na mda mwingine anataka kuhakikisha kama kweli hizo nguvu zatoka kwa Mungu au lah.
Ni hatu ambayo usipokua na neema ya Mungu unaweza ukaishia hapa hapa maana unaweza hata ukaona ni mazingaumbwe tu na hamna ukweli wowote.


3- KUITWA


Kutoka 3:4

Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

Mungu akishaona umegeuka na unajiuliza uliza maswali kuhusu mahali ulipo kama ni sahihi na miujiza inayotendeka, yeye mwenyewe atakuita kwa jina lako.
Umpokee Yesu awe Bwana na mwokozi wa maisha yako.
Siku yako ya kwanza kuokoka ilikua niwewe kuitikia katika sauti ya Mungu alikuita kwa jina lako.
Kuitikia ndio kumkubali awe Bwana wa maisha yako na akutawale hii ndio stage ya tatu
Na wengine huishia hapa pia maana huitwa lakini hawaitikii.


4- KUACHANA NA TABIA ZA UKALE


Kutoka 3:5

Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

Baada ya Mungu kukuita hatua inayofuata ni Mungu anataka wewe uachane na tabia za ukale.
Tabia ulizokua nazo hapo mwanzo ulevi,uzinzi nk
Hivi vyote anataka uviache.
Kumbuka viatu vina ashiria utayari wako wa kwenda mahali.
Mungu alijua huyu Musa hatokubali ni kumtuma kwenda kwa wana waisrael kama hatovua viatu alivonavo saivi yani utayari aliokua nao wakati Mungu amekutana nae.
Kwahio Mungu anataka uachane na hizo tabia kwanza ili aweze kukutuma sasa kwa habari ya kazi.

Utashanga kugundua kua musa hakuvua viatu.
Kwasababu biblia nayotumia haionyeshi Musa akivua viatu
Kipengele hicho basi kinatupeleka kwenye hatua nyingine ya wito.


5- HOFU YA MUNGU


Kutoka 3:6

Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.

Baada ya Mungu kumwambia musa avue viatu alafu hakuona ushirikiano toka kwake, alichokifanya ni kujitambulisha kwake.
Mungu akianza kujifunua kwako akianza kukufundisha kuhusu yeye hii ni hatua ya kuelekea kujua wito wako.
Mungu akaanza kujitambulisha kwa musa kua yeye ni Mungu wa ibrahimu,isaka na yakobo kitendo hicho kilimfanya musa aogope.
Kumbe basi hofu ya Mungu huja pale unapomjua Mungu vizuri.


6- KUTUMWA

Kutoka 3:7

Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao

Baada ya Mungu kujua sasa hakika una hofu ya Mungu ndani yako hapo ndipo Mungu sasa ataanza kujieleza kwanini alikuitwa atakwambia wito wako na utumishi ulioko ndani yako.

Kutokana na hatua hizi usitamani kuruka nenda kwa kanuni hizi na hautajichelewesha kwa kadiri unavotamani kumjua Mungu ndio hofu ya Mungu itazidi na ndipo utumishi wako utazidi kukua

Mwisho
Ubarikiwe kwa somo hili

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers