Skip to main content

NGOME YA KUANGUSHA

2 Wakorintho 10:4
(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

Biblia inasema silaha za vita vyetu si za mwili.
Kwahio tujue mpaka hapo tupo kwenye vita
Maana hatuwezi tukawa tunaongelea kuhusu maswala ya silaha za vita wakati hatuna vita

Kwahio hapo nikukujulisha kua tupo kwenye vita.
Lakini pia ni kukujulisha kua hio vita haitumii silaha unazozijua hizi za mwili
Yani bunduki,mabomu nk

Ila zinauwezo katika Mungu,
Kwa tafsiri rahisi hizo silaha zimetengenezwa na Mungu
Na kila silaha inauwezo wake
Tunajua kuna bunduki ina uwezo wake
Kuna short gun pia kuna sniper hizi zote ni silaha lakini zinauwezo tofauti

Hivo nategemea kuona silaha hizi ambazo zina uwezo katika Mungu zinauweza wake

Na kutokana huu mstari tunajulishwa hizo silaha zinauwezo kiasi kwamba zinaweza kuangusha ngome

Ngome ni majumba yaliojengwa kwa ufasaha ambayo ukuta wake ni mgumu na ni imara sana sio rahisi uanguke

Kwahio hizo silaha zinauwezo wa kuangusha hata hizo ngome

Sasa kwa nini silaha za Mungu zinapewa nguvu ya kuangusha ngome
Kwani vita yetu ni ya kuangusha ngome au?

Na je hizo ngome zinatuzuia nini sisi mpaka tuanze kuziangusha?

2 Wakorintho 10:5
tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo

Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka
Kumbe mawazo ndio ngome inayoongelewa hapa.
Kumbe mambo yote unayowaza ni ngome unakua umeiinua

Je unawaza nini?
Sasa tukisoma juu tutazani tunatakiwa kuangusha kila ngome lakini
 je hadi mawazo mazuri tuyaangushe?

Au biblia inataka kutumbia nini?
Anaendelea kusema na kila kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu

Kumbe mawazo ambayo tunatakiwa kuyaangusha ni yale ambayo yanataka kujiinua juu ya elimu ya Mungu

Elimu ya Mungu inasema huo ugonjwa unapona
Mawazo yako yanakwambia kua huo ugonjwa hauponi ina maana hayo mawazo yanataka kujiinua juu ya elimu ya Mungu
Kwahio hayo ni ya kuangusha tu

Unajiona kua hupendwi unajihisi kua mnyonge
Wakati elimu ya Mungu inakutaka uwe hodari na Yesu anakupenda
Hayo mawazo ni ngome inayotakiwa kuangushwa

Sasa ukishaangusha hayo mawazo
Kuna tendo la kigaidi unatakiwa kulifanya
Nalo ni tendo la utekaji

Unajua fikra zako zinagombaniwa na pande mbili
Kwa shetani na kwa Mungu
Lazima utumie silaha za Mungu kuteka fikra zako
Ukiteka mtu ujue yuko chini ya uangalizi wako na atafanya yote unayomwambia

Kwahio lazima uteke fikra zako na kuziamuru zimtii Kristo
Tumia silaha za Mungu kuteka fikra zako zimtii Kristo
Vita kubwa mtu hua anapitia nayo ni ya kwenye mawazo
Kwa sababu mawazo hujenga ngome
Sasa ni kitu gani unawaza

Anza kuangusha kwanza mawazo mabaya
Alafu ziteke fikra zako zimtii Yesu

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers