Skip to main content

NYARAKA ZA YEZEBELI part 1



NYARAKA ZA YEZEBELI
1 Wafalme 19:2-3
Ndipo Yezebeli akampelekea Eliya mjumbe, kusema, Miungu wanifanyie hivyo na kuzidi, nisipokufanya roho yako kesho, panapo wakati huu, kama roho ya mmojawapo wa hao.
Naye alipoona hayo, aliondoka, akaenda aihifadhi roho yake, akafika Beer-sheba, mji wa Yuda, akamwacha mtumishi wake huko.

neno nyaraka sio geni
Nyaraka ni documents
Documents zilizoandikwa jambo husika

Biblia ni nyaraka tofauti tofauti za watumishi wa Mungu zizlizoletwa pamoja

Nyaraka za yezebeli
Ni nyaraka au documents ambazo anaziandika yezebeli


Umuhimu wa nyaraka

Wewe unaweza kua dereva mzuri sana
Na traffick anaona kabisa unaendesha vizuri wala huendi kinyume na sheria za barabarani
Lakini akikusimamisha afu akagundua hauna driving license
Kwa kweli hapo hapo utapigwa fine
Ina maana documents ni muhimu sana
Nyaraka ni muhimu sana

Ni kutolee mfano wa kiroho
Yesu alipojaribiwa
Alimshinda shetani kwa nyaraka
Alikua anasema imeandikwa
Imeandikwa
Ina maana kama hayo alikua anasema Yesu yasingeandikwa Yesu asingeweza kuyatumia

Yesu kwa kutumia neno lililoandikwa
Au kwa kutumia nyaraka
Aliweza kumshinda Shetani


Sasa kuna nyaraka za Yezebeli


1 Wafalme 19:2

Ndipo Yezebeli akampelekea Eliya mjumbe, kusema, Miungu wanifanyie hivyo na kuzidi, nisipokufanya roho yako kesho, panapo wakati huu, kama roho ya mmojawapo wa hao.

Huyu ni yezebeli kapeleka ujumbe kwa eliya
Baada ya eliya kuua manabii 400 wa baali kwa kuwakata vichwa
Yezebeli kamtumia mjumbe kua atamuua kama vile alivowauwa hao manabii

1 Wafalme 19:3

Naye ALIPOONA hayo, aliondoka, akaenda aihifadhi roho yake, akafika Beer-sheba, mji wa Yuda, akamwacha mtumishi wake huko.

Biblia inasema nae alipoona

Yani haijasema aliposikia
Inasema alipoona
Inamaana ujumbe uliletwa ulikua kwa maandishi
Ina maana yezebeli alimtuma mjumbe akampa barua inayosema hayo maneno

Sasa turudi nyuma taratibu
Kama yezebeli alitaka kumuua eliya kwanini alimtumia barua kwanza
Kwanini asinge mwambia yule mjumbe kamuue eliya?

Pili biblia inasema eliya alipoona hayo aliondoka kuhifadhi roho yake
Tujiulize nabii mkubwa kama eliya aliweza kuua manabii 400  yeye peke yake kwanini ametishwa na ujumbe unaotoka kwa mwanamke mmoja tu?

Kutokana na maswali hayo
Nataka nikujulishe kitu hichi siku ya leo
Kila kinachokutokea lazima kiwe kimeandikwa

Chochote unachopitia leo kimeandikwa mahali

Eliya alikimbia kwasababu alijua kitu kikishaandikwa lazima kitokee
Yeye kama nabii anajua nguvu ya maandishi anajua nguvu ya nyaraka

Wote tunajua eliya alipaa kwenda mbinguni
Ni kweli
Ila leo nitawaonyesha sehemu eliya anakatwa kichwa ili kutimiza yale yalioandikwa juu yake na Yezebeli


Marko 9:11

Wakamwuliza, wakisema, Mbona WAANDISHI hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?

Wanafunzi wa Yesu wakamwuliza Yesu mbona waandishi
Soma vizuri inasema mbona waandishi
Hunena ya kwamba imempasa eliya kuja kwanza

Ilikua imeandikwa kua lazima eliya japo amepaa mbinguni lazima arudi tena

Sasa tutaona Yesu alichojibu
Marko 9:12

Akajibu akawaambia, Ni kweli Eliya yuaja kwanza, na kurejeza upya yote; lakini, pamoja na haya, AMEANDIKIWAJE Mwana wa Adamu ya kwamba atateswa mengi na kudharauliwa?


Yesu akasema ni ukweli lazima eliya aje kwanza na kurejesa upya yote

Lakini akasema pamoja na hayo
Ameandikwaje mwana wa adamu
Kumbe hata mateso aliyopitia Yesu ni kwasababu ilikua imeandikwa
Lakini Yesu hakuishia kusema tu yale yalioandikwa juu yake

Marko 9:13

Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtenda yote waliyoyataka kama alivyoandikiwa.

Akasema eliya ameshakuja
Na wamemtenda yote kama alivyoandikiwa

Ina maana eliya yale aliyoandikiwa ndo wametenda
Na alichoandikiwa ni kua atauliwa kwa kukatwa shingo ama alivowakata wale manabii baali

Somo linaendelea na tutajua jinsi eliya alivorudi....

Mubarikiwe wote

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers