Skip to main content

NYARAKA ZA YEZEBELI part 2

NYARAKA ZA YEZEBELI


Inaendeleaa....


Sasa napenda kuendelea pale nilipoishia kwenye hili somo letu, nataka niwekee msisitizo zaidi kwenye eneo la nyaraka

Mathayo 2:4

Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

Herodi alisikia Yesu kazaliwa
Ila hakujua kazaliwa wapi
Ila kwasababu anaufahamu wa mambo ya kiroho
Akakusanya makuhani
Na waaandishi wa watu
Akawauliza Kristo kazaliwa wapi?

herodi alijua kama kristo kazaliwa lazima hata sehemu aliozaliwa lazima iwe imeandikwa kua atazaliwa wapi
Maana anajua kila kitu lazima kiandikwe kabla hakijatimia

Mathayo 2:5

Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

Wakajibu wakasema bethlehemu kama ilivyoandikwa

Kumbe walijua kabisa Yesu atakua bethelehemu kwasababu imeandikwa hivo

Kazi moja wapo ya Yezebeli ni anahusika na nyaraka
Ukiona wewe unapita katika hali ya umasikini ujue Yesebeli kuna barua ameandika juu yako kua wewe ni masikini
Kitu chochote shetani anachotaka kikutokee katika maisha yako lazima yezebeli akiandike kwanza

🌹Kwanini nasema yezebeli
Nitakupa mfano mwingine wa yezebeli alivoandika nyaraka

1 Wafalme 21:7-9

Yezebeli mkewe akamwambia, Je! Sasa wewe unaumiliki ufalme wa Israeli? Ondoka, ule chakula, moyo wako ufurahi; mimi nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.
Basi, akaandika nyaraka kwa jina la Ahabu, akazitia muhuri yake, akazipeleka zile nyaraka kwa wazee, na kwa watu wenye nguvu waliokuwa katika mji wake, waliokaa pamoja na Nabothi
Akaandika katika zile nyaraka, akasema, Pigeni mbiu ya watu kufunga, mkamweke Nabothi juu mbele ya watu,

Alitaka nabothi auliwee
Kwahio kama kawaida yake alijua nguvu ya nyaraka

Na saivi akatumia jina la ahabu hakutumia jina lake

Inamaana shetani akitaka ufukuzwe kazi
Upewe barua ya termination
Yesebeli yeye ndo ataandika hio barua afu atatumia tu jina la boss wako
Kwahio unavopokea ile barua unazani ni boss wako kaandika kumbe ni roho ya yezebeli ilimvaa

Kwanini nyaraka zako muhimu hua zinakua shida kupatikana kwasababu roho ya yezebeli inazuilia hizo nyaraka

YESU ALIKUJA KUFUTA NYARAKA ZOTE ZILIZOANDIKWA JUU YAKO

 Moja ya shughuli aliokuja kufanya Yesu ni kushughulikia nyaraka za Yezebeli
Yesu alikuja kuifuta hati ilioandikwa
Na kuigongelea msalabani

Wakolosai 2:14

akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Kwahio moja ya kazi alizokuja kufanya Yesu ni kushughulikia vyote vilivoandikwa juu yetu na yesebeli ili visifanye kazi kwetu
Lakini usipokua na uelewa huo bado hizo nyaraka za yezebeli zitafanya kazi juu yako


ELIYA AMESHARUDI NA WAKAMFANYA VILE WALIVOANDIKA JUU YAKE


Wote tunajua elia alipaa mbinguni si ndo hivo
Na kati ya watu wa kwenye biblia unaweza kusema hawakufa unaweza kumtaja elia kama mmoja wao

Kwa namna hio unaweza kusema kwa kua eliya alipaa mbinguni basi nyaraka ya yezebeli haikufanya kazi
Lakini ebu tusome maandiko

Malaki 4:5

Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya.

Katika kitabu cha malaki kinasema kua Mungu atamleta nabii eliya kabla siku ya Bwana

Biblia ikisema kabla siku ya Bwana ujue inamaanisha kabla ya Yesu

Kwahio eliya alitakiwa aje kabla ya Yesu


Swali je Eliya alikuja kabla ya Yesu?

Mathayo 17:11

Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,

Yesu huyu akawaambia wanafunzi wake ni kweli kua eliya atakuja wa kwanza naye atatengeneza yote

Mathayo 17:12

ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.

Akasema ila ameshakuja japo wengi hawajamtambua
Kama wengi leo ambavo hawajamtambua elia alivokuja

Mathayo 17:13
Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.

Ndipo wanafunzi walipofahamu aah kumbe ni yohana mbatizaji

Kumbe eliya ndo yohana mbatizaji

Wakati malaika anamtokea zakaria baba yake yohana haya ndio maneno alimwambia

Luka 1:17

Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.

Yohana atatembea katika roho ya eliya
Inamaana eliya alikua katika mwili wa yohana
Anaeonekana kua ni Yohana mbatizaji agano jipya ndio eliya

Je kifo cha Yohana ni kama alivoandikiwa Eliya?

Mathayo 14:10

akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani.

Ndio maana nyaraka ni muhimu
Nyaraka alioandikwa elia kua atauliwa kama alivowauw wale manabii 400
Maana aliwakata kichwa ndivyo alivouawa alivokuja kwa mwili wa yohana

Sasa kazi kwako kufuta na kuharibu kila nyaraka zote zilizoandikwa juu yako

🌹🌹Na nikwambie kitu yezebeli ni roho ambayo haijali unaupako kiasi gani
Kama yezebeli hakumuogopa eliya na ule upako wake wote hatukuogopa wewe kwa kukuandikia nyaraka
Na nisema tufurahi maana nyakati tulizopo ni za neema Yesu alishagongelea msumari  nyaraka zote msalabani tumia nguvu ya msalaba kujipatia ushindi.

Ubarikiwe kwa somo hili.

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers