Skip to main content

TOFAUTI YA ROHO NA MWILI

Mwanzo 1:26
Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu,kwa sura yetu
Hii lazima ikupe maswali kua Mungu anafananaje?

Biblia inatupa majibu kua Mungu anafananaje.

Yohana 4:24
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli


Biblia inasema Kua Mungu ni roho
Hivo basi Mungu akisema tumfanye mtu kwa mfano wetu na kwasura yetu basi hapo tunajua kua Mungu anamfanya mtu ambae ni roho na yeye

Ila huyo mtu ambae ni Roho kuna dhumuni kuu aliloumbiwa

Aliumbwa ili atawale, Mungu baada ya kuumba kila kitu akataka mtawala na huyo mtawala alitaka afanane nae
Kwahio Mungu akamfanya mtu ambae ni Roho

Mwanzo 1:27
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

Mungu akaumba mtu kwa mfano wake
Mwanaume na mwanamke
Hii ni siku moja
Kwahio mwanamke na mwanaume waliumbwa siku moja katika Roho
Na hakusema Roho moja awe msaidizi wa mwingine lakini wote kwa pamoja aliwaumba kwa ajili ya kutawala

Lakini usisahau kua walioumbwa kwa ajili ya kutawala ni wale wa Rohoni

Baada ya Mungu kuumuumba mwanamme na mwanamke katika Roho
Alifanya yafuatayo

Mwanzo 1:28
Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Mungu akawabariki
Usisahau baraka hizi zinakwenda kwa mtu wa Rohoni
Akawaambia zaeni,mkaongezeke,wakatawale na mambo yote ya kimamlaka walipewa

Ila walipewa watu wa rohoni

Sasa katika Sura ya pili ya kitabu cha mwanzo tunaona sasa Mungu sasa akimuumba mtu katika mavumbi na huoni akisema tumfanye mtu kwa mfano wake maana huo haukua mfano wake

Mwanzo 2:7
Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Ila Siku anapomuumba mtu katika mwili alimuumba mmoja tu ambae ni mwanaume
Ina maana sada roho ya mwanaume ilipata mwili tayari kwahio mwili ukakutana na Roho

Sasa utashangaa kuona Mungu maagizo aliyoyatoa kwa adamu pale alipokamilika katika mwili na Roho

Mwanzo 2:15
Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.


Mungu hakupoteza mda kuanza tena kubariki na mwili wa adamu
Chap chap akaupatia kazi
Akamuweka kwenye bustani afu akamwambia alime na aitunze

Lakini kama haitoshi Mungu akampa na masharti huyu mtu

Mwanzo 2:17
walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

Akamuonya usile tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya maana siku atakayo kula hakika atakufa

Yani ile siku atakayokula lile tunda siku hio hio ndo atakufa.

Hii inaonyesha kwanza kua mtu wa Rohoni sio rahisi kumtamanisha uovu
Ila mwili ni dhaifu mahali popote panapohusisha jambo kimwili lazima kuwe na mipaka

Ndio maana Maagizo aliopewa mwanamke na mwanamme wakati wako rohoni ni tofauti na pale adamu alivokuja katika mwili

Roho iko radhi kutenda mema lakini mwili ndio unaosababisha udhaifu

Na Mungu kwa kujua hili akampa angalizo kabisa mtu wa mwilini lakini hatuoa angalizo kwa mtu wa Rohoni

Lakini pia tofauti nyingine ni hii
Vitu vyote huanzia rohoni kwanza ndio huja mwilini
Mungu alimuumba adam na hawa kwanza Rohoni ndio akaja kuumba mwilini

Na pia jambo la mwenzako likianza kudhihirika katika mwili haimaniishi kua lako halipo ila bado tu mda wake

Kumbuka adam na hawa kiroho waliumbwa siku moja lakini kimwili kila mtu aliumbwa siku yake

Hii inamaana baraka ya mtu ipo rohoni tayari inasubiria tu wakati wa kudhihirika

Ni kweli unaweza kupokea neno la kinabii siku moja na mwenzako la mwenzako likawahi kutokea kabla ya lako
Haimaanishi kwamba halipo
Bali mda wake bado
Ubarikiwe kwa somo hili
Amen

Comments

Ni mfalme gani wa israel ambaye alifanya israel igawanyike na kua falme mbili?

ZILIZOPENDWA ZAIDI

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)

       ISAYA 28:13 "Kwa sababu hiyo neno la BWANA kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri, KANUNI juu ya KANUNI, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo......" Mungu huwa anafanya kazi kwa kutumia kanuni zake alizojiwekea ili kuyaendesha maisha ya mwanadamu Kwahiyo unapofanya maombi ni lazima uelewe kanuni za Mungu anazotumia katika kujibu maombi ya wanadamu waliopo hapa duniani. Na kanuni hizo utazipata ndani ya Neno la Mungu, mimi kama mwalimu nataka nikusaidie kukuonyesha baadhi ya kanuni hizo. HATUA NNE ZA KUPITIA MAOMBI: Katika wewe kuomba huwa hayo maombi yako ni lazima yapitie ngazi/hatua hizi { i } Ni kuomba Nilazima wewe uombe hilo ni jukumu lako. { ii } Ni Mungu kusikia maombi yako. Unapoomba hatua inayofuata ni Mungu kusikia hayo maombi. { iii } Ni Mungu kutafakari hayo maombi yako. Baada ya wewe kuomba na Mungu kutafakari, huwa hatua inayofuata ni Mungu kuyatafakari hayo maombi yak...

HASARA ZA MANUNG'UNIKO

BERNARD STEVEN B wana YESU asifiwe,  Napenda tujifunze kuhusu manung'uniko na hasara zake kwa wewe MKRISTO. Nini maana ya Manung'uniko? N aweza kusema manun'guniko ni ile hali ya kulaumu au kulalamika kwa habari ya jambo fulani na kuona kua hustahili kupitia unayopitia. M ara nyingi mtu mwenye manung'uniko ni mtu ambaye hana shukrani mbele za MUNGU, mtu wa aina hii akipitishwa kwenye majaribu kidogo tu huoni kana kwamba MUNGU hayupo na anaweza hata kutoa maneno ya kufuru mbele za MUNGU. K abla hujaanza kunung'unika kwa habari ya hayo unayopita nayo, ebu jaribu kutafakari ulipotoka na ulipo sasa. H ivi unatambua kua hata pumzi uliokua nayo ni jambo la kusema asante kwa MUNGU. H ujajiuliza tu kwanini majaribu kwako hayaishi, basi tambua mengine si majaribu bali ni adhabu MUNGU ana achilia kwako kwa kunun'gunika, tambua kua wewe si wa kwanza kupitia majaribu, wapo wengi wamepitia na wameshinda. HASARA ZA MANUNG'UNIKO  Kufa kiroho kabisa ...

KANUNI ZA KUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU.(SEHEMU YA PILI)

Shalom rafiki yangu karibu sana tena leo katika somo letu hili la kupata maarifa ya kiroho. { Sehemu ya pili } Jana nilikuonyesha kanuni tatu nataka leo tuendelee na kanuni nyingine ambazo zitamfanya Mungu ajibu maombi yako, kwahiyo ni muhimu sana kuzifanyia kazi hizi kanuni kwasababu zitafanya maombi yako kujibiwa haraka na Mungu. KANUNI HIZO ZA KUMFANYA MUNGU AJIBU MAOMBI YAKO NI PAMOJA NA: 4 Muombaji sharti uliweke Neno la Mungu kwa wingi ndani ya moyo wako.     YOHANA 15:7 "Ninyi mkikaa ndani yangu, na MANENO yangu yakikaa NDANI YENU, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"    WAKOLOSAI 3;16 "Neno la Kristo na likae au lidumu kwa wingi ndani yenu katika hekima yote"     YEREMIA 1:12 "Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema; kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize" Maombi yanayoombwa kwa msingi wa Neno la Mungu huwa yanaleta majibu ya haraka kwasababu kanuni ya Mungu huwa ni kuliangalia Neno lake na ku...

Total Pageviews

Followers