Isaya 40:31
bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Ebu vuta hisia zako uko mahali unamgojea mtu.
Afu jiulize unamgojea aje kufanya nini?
Je una appointment nae?
Kwa maswali haya tu ni dhahiri kabisa hauwezi kumngojea mtu kama hamjapanga mkutane mahali au kama hajakwambia umsubiri mahali.
Biblia inasema wamngojeao Bwana
Tujiulize kwanini unamgojea Bwana, je una appointment yeyote na yeye,
Je amekwambia umsubirie labda akuletee kitu.
Ebu tafakari unamgojea Bwana afanyaje?
Usije ukawa unamgojea wakati yeye hana taarifa yeyote kwamba unamgojea
Kwahio ili ufike hatua ya kumngojea mtu lazima pande zote mbili ziwe na taarifa
Yamkini kuna kitu umemuomba Mungu
Akasema subiri
Basi wewe unatakiwa umngojee Bwana.
Mungu akikuahidi jambo lazima ujifunze kumngojea hadi pale atakapotimiza
Ili uweze kumngojea Bwana
Sio vitu vyote ni vya kungojea vitu vingine Mungu anavifanya hapo kwa hapo kama ni wakati wake
Lakini vingine atakwambia subiri.
Utajuaje sasa kama amekwambia usubiri au lah.
Jifunze kumsikiliza.
Utajifunza kumsikiliza pale utakapokua msomaji mzuri wa neno na mtu wa kutafakari neno sana.
Neno linapokuja kwako, Mungu hulileta kama andiko na hua linabeba ujumbe ndani yake,
Huo ujumbe utaupata pale utakapoanza kutafakari hilo neno,
Huo ujumbe ndo kitu Mungu anachokusemesha.
Sasa ukishapokea huo ujumbe kama ni ahadi ya kitu atakachokutendea.
Jifunze kumngojea Bwana
Kumngojea ni kua na imani na kile ulichoahidiwa kua lazima kitimie hata ipite mda mrefu kiasi gani bado unaamini huko ndo kumngojea Bwana
Sasa faida za kuomngojea Bwana ni zifuatazo:
1- Utapata nguvu mpya
Kama kuna nguvu mpya basi ya zamani ipo, yamkini jana ulishinda misukosuko kwa sababu ya nguvu uliokua nayo jana
Haimaanishi hio nguvu inaweza kustahimili misukosuko yale
Hata wachezaje wa mpira au mchezo wowote hufanya mazoezi ili wapate nguvu mpya maana upinzani unafanya bidii kuongeza nguvu mpya kila siku
Nguvu mpya utaipata ukiwa na tabia ya kumngojea Bwana
Kwahio kumngojea Bwana ni kama mazoezi ya kuongeza nguvu
Zoezi la kumngojea Bwana litakupa nguvu mpya.
2-Watapanda juu kwa mbawa kama tai
Tabia ya kumngojea Bwana itakufanya ukue sana katika viwango kiroho na kimwili
Tai ni ndege ambae anaweza kuruka juu sanaa kuliko ndege wote.
Ina maana tabia ya kumngojea Bwana inakufanya uwe juu ya wote katika kila unachofanya
3-Watapiga mbio wala hawatachoka
Kumngojea Bwana kutakufanya uwe na speed.
Wengi huchokea njiani katika safari yao ya wokov, katika biashara zao maana wanaona walianza na mbio vizuri lakini sasa wamechoka hawaoni kwenda mbele
Kumngojea Bwana kutakupa kukimbia tu na utakimbia tu bila kuchoka
4-Watakwenda kwa miguu wala hawatazimia
Kutembea umbali mrefu kwa mda mrefu mda mwingine kutasababisha uzimie kwasababu ya kukosa nguvu
Lakini zoezi la kumngojea Bwana linakufanya uwe imara uweze kutembea umbali mrefu bila kuzimia
Nini maana ya kutembea,
Kutembea kuna ambatana na vile vitu unavofanya
Wagalatia 5:16
Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
Kuenenda kunaitaji miguu kwahio tunaposema kutembea bila kuzimia
Ni kutenda yale ya rohoni bila kuzimia yani bila kuacha.
Mungu akubariki kwa somo la leo
bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Ebu vuta hisia zako uko mahali unamgojea mtu.
Afu jiulize unamgojea aje kufanya nini?
Je una appointment nae?
Kwa maswali haya tu ni dhahiri kabisa hauwezi kumngojea mtu kama hamjapanga mkutane mahali au kama hajakwambia umsubiri mahali.
Biblia inasema wamngojeao Bwana
Tujiulize kwanini unamgojea Bwana, je una appointment yeyote na yeye,
Je amekwambia umsubirie labda akuletee kitu.
Ebu tafakari unamgojea Bwana afanyaje?
Usije ukawa unamgojea wakati yeye hana taarifa yeyote kwamba unamgojea
Kwahio ili ufike hatua ya kumngojea mtu lazima pande zote mbili ziwe na taarifa
Yamkini kuna kitu umemuomba Mungu
Akasema subiri
Basi wewe unatakiwa umngojee Bwana.
Mungu akikuahidi jambo lazima ujifunze kumngojea hadi pale atakapotimiza
Ili uweze kumngojea Bwana
- Anza kwa kumsikiliza yeye, jifunze kumsikiliza yeye
Sio vitu vyote ni vya kungojea vitu vingine Mungu anavifanya hapo kwa hapo kama ni wakati wake
Lakini vingine atakwambia subiri.
Utajuaje sasa kama amekwambia usubiri au lah.
Jifunze kumsikiliza.
Utajifunza kumsikiliza pale utakapokua msomaji mzuri wa neno na mtu wa kutafakari neno sana.
Neno linapokuja kwako, Mungu hulileta kama andiko na hua linabeba ujumbe ndani yake,
Huo ujumbe utaupata pale utakapoanza kutafakari hilo neno,
Huo ujumbe ndo kitu Mungu anachokusemesha.
Sasa ukishapokea huo ujumbe kama ni ahadi ya kitu atakachokutendea.
Jifunze kumngojea Bwana
Kumngojea ni kua na imani na kile ulichoahidiwa kua lazima kitimie hata ipite mda mrefu kiasi gani bado unaamini huko ndo kumngojea Bwana
Sasa faida za kuomngojea Bwana ni zifuatazo:
1- Utapata nguvu mpya
Kama kuna nguvu mpya basi ya zamani ipo, yamkini jana ulishinda misukosuko kwa sababu ya nguvu uliokua nayo jana
Haimaanishi hio nguvu inaweza kustahimili misukosuko yale
Hata wachezaje wa mpira au mchezo wowote hufanya mazoezi ili wapate nguvu mpya maana upinzani unafanya bidii kuongeza nguvu mpya kila siku
Nguvu mpya utaipata ukiwa na tabia ya kumngojea Bwana
Kwahio kumngojea Bwana ni kama mazoezi ya kuongeza nguvu
Zoezi la kumngojea Bwana litakupa nguvu mpya.
2-Watapanda juu kwa mbawa kama tai
Tabia ya kumngojea Bwana itakufanya ukue sana katika viwango kiroho na kimwili
Tai ni ndege ambae anaweza kuruka juu sanaa kuliko ndege wote.
Ina maana tabia ya kumngojea Bwana inakufanya uwe juu ya wote katika kila unachofanya
3-Watapiga mbio wala hawatachoka
Kumngojea Bwana kutakufanya uwe na speed.
Wengi huchokea njiani katika safari yao ya wokov, katika biashara zao maana wanaona walianza na mbio vizuri lakini sasa wamechoka hawaoni kwenda mbele
Kumngojea Bwana kutakupa kukimbia tu na utakimbia tu bila kuchoka
4-Watakwenda kwa miguu wala hawatazimia
Kutembea umbali mrefu kwa mda mrefu mda mwingine kutasababisha uzimie kwasababu ya kukosa nguvu
Lakini zoezi la kumngojea Bwana linakufanya uwe imara uweze kutembea umbali mrefu bila kuzimia
Nini maana ya kutembea,
Kutembea kuna ambatana na vile vitu unavofanya
Wagalatia 5:16
Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
Kuenenda kunaitaji miguu kwahio tunaposema kutembea bila kuzimia
Ni kutenda yale ya rohoni bila kuzimia yani bila kuacha.
Mungu akubariki kwa somo la leo
Comments
Post a Comment